Wednesday, 12 March 2025

YANGA SC Watamba Tuzo za Februari Ligi Kuu ya NBC 2024/25

  AjiraLeo Tanzania       Wednesday, 12 March 2025
WARNING
Beware of Job Scammers!
Please Never Pay Money To Get A Job!
DUBE MCHEZAJI BORA FEBRUARI LIGI KUU YA NBC 

YANGA SC Watamba Tuzo za Februari Ligi Kuu ya NBC 2024/25

MSHAMBULIAJI wa timu ya Young Africans (Yanga) ya Dar es Salaam, Prince Dube, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa mwezi Februari wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa mwaka 2024/25, huku Miloud Hamdi pia wa Yanga akichaguliwa Kocha Bora wa ligi hiyo kwa mwezi huo.
YANGA SC Watamba Tuzo za Februari Ligi Kuu ya NBC 2024/25
Prince Dube
Dube alionesha kiwango kizuri chenye mwendelezo akiwashinda Aziz Ki wa Yanga na Selemani Bwenzi wa KenGold, alioingia nao fainali katika mchakato wa Tuzo za Mwezi uliofanywa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
READ ALSO:
Mchezaji huyo alitoa mchango mkubwa kwa timu yake katika michezo saba ambayo Yanga ilicheza mwezi huo na kufunga mabao matano na kuhusika na mengine matano kwa dakika 562 alizocheza. Yanga ilishinda michezo sita na kutoka sare mmoja.

Kwa upande wa Hamdi aliyeingia fainali katika mchakato huo na Fadlu Davids wa Simba na Fred Minziro wa Pamba Jiji, aliiongoza Yanga kushinda michezo minne na sare moja, ambapo kwa mwezi huo Yanga ilicheza michezo saba.

Hamdi aliiongoza Yanga ilipotoka suluhu na JKT Tanzania, kisha ikazifunga KMC mabao 1-6, Singida Black Stars (2-1), Mashujaa (0-5) na Pamba Jiji (0-3). Mechi nyingine ambazo Yanga ilishinda mwezi huo lakini haikuwa chini ya Hamdi ni dhidi ya KenGold (6-1) na dhidi ya Kagera Sugar (4-0).

Pia Kamati ya Tuzo imemchagua Meneja wa Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo uliopo Dar es Salaam, Ashraf Omar, kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Februari kutokana na kufanya vizuri katika menejimenti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.
logoblog

Thanks for reading YANGA SC Watamba Tuzo za Februari Ligi Kuu ya NBC 2024/25

Previous
« Prev Post

No comments:

Post a Comment